
Mbali ya wakongwe hawa, Timu za
Zanzibar, Mafunzo na Jamhuri, nazo zitaingia uwanjani kwa Mafunzo
kucheza na Liga Muculmana de Maputo ya Msumbiji katika CAF CHAMPIONZ LGI
na Jamhuri kuivaa Hangwe ya Zimbabwe kwenye Kombe la Shirikisho.
Tayari Zamalek, ambao wamewahi kuwa
Mabingwa wa Afrika mara 5, wameshatua Dar es Salaam bila ya Wachezi wao
Ahmed Hassan, Muhammad Ibrahim na Salah Suleiman.
Majuzi Zamalek walicheza mechi yao ya
mwisho ya majaribio na kuifunga Telecom Egypt bao 4-1 kwa bao za Amr
Zaki, Ibrahim Hassan na Ahmad Jaffar.
Simba yaenda Rwanda bila Wachezaji kadhaa
Simba iliondoka Alhamisi jioni kwenda Kigali, Rwanda kupambana na Kiyovu huku Wachezaji kadhaa wakiachwa.
Wachezaji ambao hawakusafiri ni Gervais
Kargo, Derrick Walulya, Haruna Moshi 'Boban', Ulimboka Mwakingwe, Amir
Maftah na Hassan Khatib na imesemwa baadhi yao ni majeruhi.
Pamoja na Kocha Cirkovic Milovan na
Wasaidizi wake Amatre, Daktari Cosmas Kapinga na James Kisaka, Kocha wa
Makipa, Viongozi wengine ambao wamo kwenye msafara huo ni Makamu
Mwenyekiti Geofrey Nyange 'Kaburu', Katibu mkuu Evodius Mtawala, Fransis
Silaya (Mjumbe wa Kamati ya Utendaji).
Wachezaji waliosafiri ni:
Makipa: Juma Kaseja na Ali Mustapha 'Barthez'
Mabeki: Nassor Said 'Cholo', Juma Jabu, Juma Nyoso, Kelvin Yondan, Victor Costa na Obadia Mungusa.
Viungo: Shomari
Kapombe, Mwinyi Kazimoto, Jonas Mkude na Patric Mafisango Washambuliaji:
Ramadhani Singano 'Messi', Edward Christopher, Salum Machaku, Uhuru
Selemani, Felix Sunzu na Emmanuel Okwi.
No comments:
Post a Comment