Chelsea imethibitisha kuwa nahodha wao John Terry amepata mipasuko
kwenye mbavu zake na watakuwa wakifuatilia hali yake kwa karibu kabla ya
mechi zinazofuata. Terry alitoboa siri jana kuwa anapata shida
kupumuaa wakati anacheza,baada ya kuumia katika mechi ya kwanza na
Benfica wiki ilyopita ila alimudu kucheza dakika zote 90 jumamosi
iliyopita katika mechi ya ligi kuu dhidi ya Aston Villa.Lakini katika
mechi ya Uefa jumatano alidumu uwanjani kwa dakika 60 tu na baadae
alitolewa. Asubuhi ya jana alhamisi vipimo vya scan vilionesha kuwa
Terry amepasuka mbavu mbili.Katika taarifa iliyotolewa kwenye mtandao wa
klabu wa www.chelseafc.com
Chelsea wamesema wamefanikiwa kulishughulikia tatizo na watamwangalia
mlinzi wao huyo wa kutegemewa kwa ukaribu zaidi kabla ya mechi
zinazofuata
No comments:
Post a Comment