Subscribe:

Ads 468x60px

VYOMBO VYA HABARI VINATENGENEZA MAAFA-UBUNIFU WETU

NAFUNGUKA KAMA HIVI NATANGULIZA SAMAHANI KAMA NITAMKERA MTU KWA NAMNA MOJA AMA NYINGINE
Ni kuhusu hivi vyombo vya habari vya Tanzania na ujinga ujinga wao unaosababisha maafa bila wao kujua.Media za kibongo zinachangia kwa kiasi kikubwa maadili kuvunjwa na pia zimekaa kiugombanishi gombanishi tu!!!
Naanzia kwenye hii ishu iliyopo kuhusu Lulu kuwekwa hatiani akihusishwa na mauaji. Hivi unadhani Lulu angekuwa kama alivyo kama sio upumbavu wa waandishi uchwara wa habari ambao wanasahau kuwa udaku ni tofauti sana na umbea…..umbea unaweza kusababisha vita maana mnajikuta mnaandika andika tu ujinga na sisi watanzania tunashangilia….binafsi huwa siogopi kitu kama nina poiti ya kujitetea haya Magazei ya Global publishers, ondoa gazeti la Uwazi, kila gazeti lilikuwaga bize kweli kumsakama Lulu, mara Lulu kafikisha miaka 18 sasa, mara amevalishwa pete ya ndoa…magazeti haya yakamvimbisha kichwa Lulu akajiona yeye ndo kila kitu hapa Tanzania.
Ni haya haya magazeti yalisababisha huyu mtoto ashindwe kufanya mtihani wa kidato walau cha nne maana sina uhakika kama wa kidato cha pili alifaulu. Yeye mwenyewe hata kama hakusema alijua kuwa magazeti yataandika LULU NDANI YA CHUMBA CHA MTIHANI, kwani Lulu kufanya mtihani nayo ni habari ya kuandika ama, hao hao watamaliza wataandika LULU APATA ZERO…kama vile hakuna vitu vya kuandika katika kurasa za mbele bwana…magazeti yakamsifu Lulu amekuwa mtu mzima naye akaanza kufanya mambo ya kiutu uzima, hayohayo magazeti yakawa yanashabikia. Haya na sasa yupo matatani yatajidai kuwa yalimuonywa.
Huu ni ujinga Zamaradi mketema katika kipindi cha Take one, anaandaa kipindi mara anamuita Jackline Wolper sijui, anamuuliza maswali ya kinafiki nafiki tu ilimradi awakere maadui zake sasa sijui hapo ndo huyu mwendesha kipindi alikuwa anakuza vipaji ama vipi, alinikera na sikumuelewa. Juzi tena kama usingekuwa msiba wa Steven Kanumba kuna jingine lilikuwa linakuja kushika katika Media, yaani Wema huyu dada wala simsifii kuwa eti ana tabia nzuri ama la…binafsi huwa hanifurahishi lakini kwa juzi hiyo huyo mtangazaji aliniacha hoi na katiuka kero kubwa…..ni katika kipindi cha EATV Friday night live, Wema kaja kwa ajili ya kutangaza filamu yake mpya lakini yule presenter akaanza kumuuliza juu ya uhusiano wake na Diamond, jamaa alinikera na nilimwona mshamba kabisa.
Sasa shida yake sijui alitaka Wema amtukane Diamond ama, sasa akishamtukana halafu Diamond akasirike amtafute mtaani ampige aue we presenter ndo kazi yako itakuwa imetimia au???? Uliboa ile mbaya..
Magazeti haya ya Shigongo haya…yakakazana kuandika ooh!! Dude kazaa na Uwoya. Hivi Dude na Ndikumanaq wakitoana roho kwa ujinga mnaotuandikia, sasa mwatufurahisha nini kwa mambo hayo ya chumbani?? Sikatai kuandika udaku lakini mnaandika umbea nyie. Mnawafanya wasanii wetu wawe juu ya maisha yao ya kawaida. Na nyie wasanii wengine ni washamba tu tena sana nasema, utakubalije kijinga jinga tu kuwa unaandiukiwa mambo yako ya ndani magazetini. Tujifunze ulaya, ambapo huwezi kumkuta Jigga=Jay Z ama Beyonce kaandikwa kijinga jinga. Sheria za uandishi haziruhusu mambo hayo ya kuandika idadi ya shanga kiunoni mwa Jokate ama chupi ya Uwoya. Hayo mnaandikiwa mnacheka.
Na wewe Wema nasikia kuwa huwa unazitafuta skendo maksudi, hala hala nakwambia ngoja uendelee na huo ushamba na ujinga halafu itakuja skendo kubwa ambayo haujaitafuta na hautaisahau kamwe, si unajidai kuona sifa unavyoandikwa andikwa. Haya magazeti haya sio kabisa yanakusifu leo kesho yanaponda.
Hawa Clouds media hawa tena yaani huwa siwaelewi kabisa wakati mwingine. Yaani wapo wanaume lakini wakati mwingine naamini wameambukizana tabia na wote kuwa wambea na wanafiki. Wanakuza mabifu hovyo hovyo halafu baadaye magazeti yanawasaidia. Mfano bifu la ROMA na huyu IZO business, kijingajinga eti kweli wapo katika ugomvi, hivi wakichomana visu ndo mwanze kuweka vipindi vya kuwakumbuka ama.
Bila media hizi hakika Lulu hadi leo angekuwa na staha asingekuwa kama alivyo. Media zimemponza Lulu halafu sasa zimemsaliti!!!! Kwa hiyo tusikae kupiga kelele Lulu Lulu, tupigie kelele na hivi vyanzo.
Mnaanzisha mashindano ya imba, vaa na cheza kama Rihanna halafu wakishavaa mnawapiga mapicha hayo mnaweka kwenye front pages za magazeti yenu. Huo ni ujinga!!!!!!
Nimeandika haya nikiwa nimekereka kabisa hasa hasa na gazeti la Sani ambalo ni kama limetoa toleo maalum kumuhusu marehemu, ukilisoma utadhani wa maana kumbe mapimbi tu…….wanaunda mabifu huku kuyazika hawajui BINAFSI NAUNGANA NAWE KAKA,KAMA UDAKU TUNAANDIKA SANA LAKINI HUU UMEPITILIZA!!!!

No comments:

Post a Comment